NJOO... MAMA HAYUPO BOOK 1 EPISODI 01

BY D.G.LWASYE ‘GIFT KIPAPA’
WHATSAP: +255 715 557 191
Tafadhari heshimu kazi ngumu ninayofanya, huruhusiwi kunakili na kupost simulizi yangu katika website, page wala whatsap group lako, stori zangu zote zimesajiliwa matumizi yoyote ya simulizi hii  bila idhini ya Gift kipapa ni kosa kisheria. 
MWANZO WA STORI:
Mtaa ulikuwa kimya ndege tu ndio waliosikika wakiiimba kila upepo ulipovuma , gari moja la kifahari lilikatisha katika mtaa huo na kuyafanya majani ya miti yaliyokuwa yamedondokea barabarani yapeperuke kimo Fulani gari hilo lilipopita majani hayo yalidondoka chini tena.
 Na harafu ukimya ulitanda tena . kando kando ya bara bara hiyo kulikuwa na nyumba za kifahari zilizozungushiwa kuta nene, pamoja na bustani za maua mazuri ya kupendeza.
Dakika kumi na tano baadae bajaji iliiibuka katika mtaa huo ilkwenda mwendo waka kasi , japo haikuwa kasi kama ile ambayo lilipita lile gari, nyumba ya kwanza ya pili ya tatu , bajaji hiyo ilipunguza mwendo , na kisha huyu mvulana aliyekuwa amevalia ovaloli lililoandikwa clean!  Clean! Alishuka , bajaji hiyo iliondoka na yeye alipiga hatua kusogelea geti kubwa lililokuwa  mbele yake.
Alibonyeza kengele na kusubiri kwa sekunde kadhaa kisha sauti kutoka kwenye kipaza sauti cha kengele hiyo ilisikika.
“jina lako nani?na ni nini kimekuleta hapa?”
Ilisikika sauti ya mwanamke .
“shadrack , natoka katika kampuni ya usafi , clean clean.”
Aliongea mwanume huyo.
“oh shadrak ! ingia nilikuwa ninakutarajia.”
Aliongea m,wanamke huyo na kihs geti lilifunguka lenyewe , shadrack aliiingia na kisha geti hilo lilijifunga.
Nyumba hiyo kubwa iliyokuwa na bustani nzuri ilimfanya shadrack astaajabu kwa dakika kadhaa.
Alipiga hatua kuelekea ulipomlango wa kuingilia ndani , na kmwkwenye mlangio huo kulikuwa na mwana mama wa makamu , aliyekuwa anamsubiri .
‘nilifikiri watawatuma wawili , utaweza kufanya kazi zote opeke  yako?”
Aliuliza mwanamke huyo huku akimuangalia shadrack usoni.
“ndio maana wamenituma mwenyewe.”
Aliitikia shadrack, huku akimuangalia mwana mama huyo usoni mara baada yta kufika pale aliposimama , macho yao yaligongana na uso wa mwanamke huyo ulikuwa na tabasamu lililofifia.
“sawa shadrsk , nataka kuuona uhodari wako , stoo  ipo kwule kwenye nyumba ya nje mlango wa tatu hii ni funguo yake , utaopata vuifaa vyote unavyohitaji.’
Aliongea mwana mama huyo.
“ahsante bibie.”
Shadrack aliitikia huku akipokea funguo hizo.
Alitembea kuelekea kwenye nyumba ya nje iliyokuwa umejitenga kwa umbali Fulani  hivi toka ilipo nyumba kubwa , nia ya kuelekea huko ilikuwa imesakagfiwa kwa zege huku pembeni kukiwa na viwanja vyenye nyasi zilizokatwa vizuri  na mwanaume ambae alikuwa akishughulika na mashine ya kukatia nyasi upande huo wa nyumba ya nje , mashine yake ilikuwa ikipiga kelele lakini mwanaume huyo alikuwa amezoea .
Upande mwingine kulikuwa na mpira wa maji uliokuwa umefungwa kifaa cha kumwagilia kilichokuwa kikirusha maji kwenye majani hayo kila upande zamu kwa zamu.
Shadrack alipofika kwenye nyumba hiyo alisogelea mlango alioelekezwa na kufungua , alipoingia ndani alijikuta anastaajabu, kila kifaa kinachotumika kwaajili ya usafi kilikuwa humo , kuna baadhi ya vifaa hata ofisimni kwao havikuwemo, kwa kweli hakuamini vifaa bora kama hiovyo vinawea kufungiwa ndani kusubiri kufanya kazi ya nyumba moja kwa muda wote huo , kila kifaa alichokiona humo kilikuwa ni ndoto ya mfanya usafi yoyote ulimwenguni hata bosi wake alikuwa akiviota vifaa hivyo.
 “unahitaji msaada?”
Ilisikika sauti hiyo iliyomshtua shadrak. Aligeuka haraka kumuangalia mtu aliyeongea .
Alikuwa ni yule mwanaume aliyemuona kwambali akikata nyasi na mashine.
“oh , Mungu wangu umenishtua.”
Aliongea shadrack na kumuangalia mwanume huyo usoni.
Mwanaume huyo alimuangalia nae pia.
‘mambo , naitwa shadrack.”
Aliongea shadrack.

“safi shadrack , vipi unahitaji msaada?”


No comments:

Post a Comment