Hakuna aliyejua sababu ya kengele hiyo kulia si kilanja mkuu
wala mgonga kengele mwenyewe yeye alifuata amri tu aliyopewa na mkuu wa shule.
Ni Joel pekee ndio alikuwa ana hisi hisi tu kwamba huenda
ujumbe wake umemfikia mkuu wa shule.
Wanafunzi wote walijipanga kila kidato na mstali wake ,
walikaa kimya ilikujua kinachoendelea.
Jukwaani alisimama mkuu wa shule na mwalimu wa taaluma,
muonekano wa mkuu wa shule uliwatisha wanafunzi wote, uso wake ulikuwa
umekunjamana kwa hasira. Jambo hili lilimfanya joel apate uhakika kwamba sasa
ujumbe wake umefika.
Kilanja mkuu aliitwa na kukabidhiwa karatasi awasomee wenzake kilichoandikwa katika
karatasi hiyo, alianza kusoma.
“kwako mkuu wa shule , shikamoo, mimi ni mwanafunzi wako
naleta malalamiko yangu juu ya jambo alilotendewa mwanafunzi wa kidato cha
kwanza katika mashindano ya kumtafuta mwanafunzi anayeweza kujieleza vizuri
katika mdahalo kwa lugha ya kiingereza.
Grace Samson mwanafunzi wa kidato cha kwanza amejieleza
vizuri sana na ametoa hoja ambazo kama angepewa nafasi ya kuiwakilisha shule
yetu katika mashindano hayo nje ya shule nina hakika angeweza kuleta sifa
ambayo kwa hakika shule yetu ingejivunia kuwa naye, lakini kwa kuwa majaji wa
shindano hilo walikuwa ni wanafunzi wa kidato cha nne basi wameamua kufanya
maamuzi wanavyojua kwa kumpatia mwanafunzi mwenzao wa kidato cha nne aitwaye
fatuma Abdalla nafasi hiyo wakati hana uwezo mkubwa kama ilivyo kwa Grace
Samson.
Nimesikitishwa sana
na maamuzi haya mkuu, na nina hoji kwamba kuna haja gani ya wanafunzi wa kidato
cha kwanza kuwekwa kwenye mashindano hayo kama watasimama kama vivuli tu?
Si kawaida kwa shule zetu hizi za serikali ambazo wanafunzi
wake wengi wanatokea shule zetu za msingi ambazo zinatumia lugha ya Kiswahili
kama lugha ya kufundishia kuweza kuzungumza na kujieleza vizuri lugha ya
kiingereza kama ambavyo Grace Samson
ameweza , bali wengi wanakuwa wakitatizwa na lugha hiyo mpaka kufikia kidato
cha pili hadi cha tatu hivi, lakini leo hii mwanafunzi wa kidato cha kwanza
ameonyesha uwezo huo na alichoambulia ni kuvunjwa moyo na kupokonywa haki yake.
Ni hayo tu mkuu nimeandika kwako kwa kuwa najua wewe ndio
mkuu wa shule hii na ndio mwamuzi wa mwisho katika masuala yote yanayoendelea
katika shule hii ili uweze kuliangalia jambo hili na kuhakikisha haki
inatendeka, Ahsante.”
Alimaliza kusoma kilanja mkuu.
Wanafunzi wote walishikwa na bumbuwazi huku wote wakiwa
wamegeuza vichwa vyao kumuangalia Grace kwani kila mmoja aliamini Grace ndio
aliyeandika barua hiyo.
“Ni nani aliyeandika barua hiyo?”
Aliuliza mkuu wa shule , wanafunzi wote walibaki kimya
“narudia tena swali langu , ni nani ameandika barua hiyo?”
Aliuliza tena mkuu wa shule macho ya wanafunzi wote yalikuwa
kwa Grace.
“mimi ndio nimeandika.”
Sauti hiyo iliposikika wanafunzi wote waligeuza vichwa vyao
kumuangalia mtu aliyeitoa kauli hiyo,
hakuna aliyeamini baada ya kumuona Joel akijitokeza.
“Ni Joel!, jamani mungu wangu!”
ilisikika sauti ya msichana mmoja aliyeongea kwa masikitiko, kwani walichoamini wanafunzi wote ni kwamba Joel amefanya kosa kubwa. Ambalo linaweza kumfanya afukuzwe shule au kupewa adhabu kali. Walifikiria hivyo kwa sababu walimfahamu vyema mkuu wao wa shule, alikuwa hapendi mzaha hata kidogo, alikuwa haoni hasara kumfukuza shule mwanafunzi hata kama akifanya kosa hata kidogo, kesi ikimfikia yeye tu basi hakukuwa na msamaha.
ilisikika sauti ya msichana mmoja aliyeongea kwa masikitiko, kwani walichoamini wanafunzi wote ni kwamba Joel amefanya kosa kubwa. Ambalo linaweza kumfanya afukuzwe shule au kupewa adhabu kali. Walifikiria hivyo kwa sababu walimfahamu vyema mkuu wao wa shule, alikuwa hapendi mzaha hata kidogo, alikuwa haoni hasara kumfukuza shule mwanafunzi hata kama akifanya kosa hata kidogo, kesi ikimfikia yeye tu basi hakukuwa na msamaha.
Wapo wanafunzi waliofukuzwa kwa kutovaa tai, soksi na hata
kutochomekea shati sembuse yeye ambaye alifikia hatua ya kumuandikia barua
kabisa.
Joel aliyajua yote hayo lakini tayari alikuwa ameshaamua
kujitoa mhanga, alikuwa tayari hata kufukuzwa shule lakini sio kuiona haki ya
Grace inapotea.
Alijitokeza mbele ya jukwaa, wanafunzi wote walikuwa wakimuangalia
kwa huruma. Upande wa Grace ndio machozi yalikuwa yakimbubujikka mashavuni ,
aliumia kuona mtu anataka kufukuzwa shule kwa sababu yake.
Mkuu wa shule alimuangalia Joel na kisha kutoa tabasamu
usoni mwake na tabasamu hilo lilikuwa la kwanza tangua aliposimama katika
jukwaa hilo ahsubuhi hiyo.
“mpigieni makofi.’
Mkuu wa shule aliamrisha, nukta hiyo hiyo wanafunzi wote
walipiga makofi huku wakiwa hawaelewi kwa nini mkuu kawambia wafanye hivyo.
“Vizuri.”
Mkuu wa shule aliongea mara baada ya wanafunzi kumaliza
kupiga makofi hayo.
Alikaa kimya kwa nukta kadhaa na kisha kuanza kuongea tena.
“huyu ni mfano wa kuigwa , katika shule yangu hajawahi
kutokea mwanafunzi mwenye ujasiri na mpenda haki kama ilivyo kwa kijana huyu.”
Aliongea huku akimuangalia Joel usoni alimpa mkono na Joel
aliupokea mkono huo na wakasalimiana kwa mara ya kwanza na mkuu wa shule tangu
aanze masomo yake miaka mitatu iliyopita.
“hongera sana kijana kwa ujasili wako.”
Aliogea mkuu wa shule huku bado wakiwa wameshikana mkono.
“ahsante mkuu.”
Aliitikia Joel japo wasi wasi bado ulikuwa haujatoka mwilini
mwake.
Mkuu wa shule baada ya kumaliza kupeana mkono na Joel,
aliwageukia wanafunzi , ambapo aliwaita majaji wa shindano hilo na kuwakaripia
sana , alimgeukia mwalimu wa taaluma naye pia alimkaripia kwa kuacha tukio
kubwa kama hilo lifanywe na wanafunzi
wenyewe japo yeye alijitetea kwamba alikuwa na dharula iliyompelekea kutofika
kabisa shule siku hiyo.
Hakuishia hapo uongozi wote wa wanafunzi ulikaripiwa
mno. Alimuita Grace mbele akampa pole na
kisha akataka pambano hlo lirudiwe muda huo huo na yeye akiwepo, vipindi pamoja
na shuguli zote za kiofisi zilisimamishwa kwa muda kisha alitaka wanafunzi wote
, walimu pamoja na wafanyakazi wa shule wote wepo katika mpambano huo.
Yani ilikuwa kama baraza la shule ambalo huwa linafanyika
mara moja tu kwa muhula.
UNATARAJIA NINI KATIKA MPAMBANO HUU WA KIHISTORIA KUWAHI
KUTOKEA KATIKA SEKONDARI TUKUYU?

No comments:
Post a Comment