NJOO... MAMA HAYUPO BOOK 1 EPISODI 08

RUDI NYUMA EPISODI YA 07

Shadrack aliwaangalia huku akitikisa kichwa chake , hakupenda lolote kati ya hayo, maisha ya washua yalikuwa yamemuingia kichwani  alikuwa anatamani kama siku moja angeamka na maisha yake yote yawe huko , alikuwa anapenda vile vicheko vyao, mandhari tulivu  muziki wa taratibu kutoka katika piano inayobonyezwa na mtaalamu wa muziki pamoja na  yale maglasi ya wayne wanayo yashikikilia wakiwa wamekusanyika pamoja kwenye sherehe zao , waliziita dina parti , valentine na majina mengine kibao ya kitasha kibao , shadrack alikuwa akiota hivyo vitu kila siku lakini kitu pekee alichokuwa anakipata ni hizi nyimbo za kina dogo mfaume na kazi yake ya dukani pamoja na zingine zingine walizotwanga wakina omari omari na  waimba singeli kibao, pamoja na hivi vihoja vya watu kuvua nguo hadharani kama wehu, bila kujari watoto wadogo kuwepo jirani , wenyewe waliita kumwaga razi na kweli radhi ilikuwa inamwagika sio mchezo.
“eeeeh , shadrack, jamaa yangu leo nimekuotea, uniambii kitu.”
Shadrack aliisikia sauti hiyo  na kugeuka kumwangalia mtu aliyemuita , alikuwa ni mmoja kati ya wale wanaume waliozunguka duara  mule kirabuni.
Domo lake lilikuwa zito na alikuwa akiyumba yumba hivi kusogea jirani toka kirabuni kumfuata shadrack.
“potonto! kumamako walai huyu mjinga atanisumbua  kinoma , sijui hata kwa nini nimepita huku kirabuni.”
Alilaani shadrack  huku akimuangalia potonto akija  kwa kuyumba nyumba , aligonga meza kadhaa walizokaa walevi wenzake wakinywa mtungi, nusu amwage mitungi yao , chupa  pamoja na mabakuli ya plastiki yaliyokuwa na pombe hizo yalitikiska tikisika hivi kwenye meza hiyo.
“oya wewe fala angalia unakokwenda , mwangalie kwanza mwendo wake ka msenge.”
Aliropoka mmoja kati ya walevi waliokuwa wamekaa kwenye meza iliyotikiswa baada ya pombe yake kumwagika kidogo kwenye meza hiyo.
“ndio ni msenge fresh namfila na mkeo vile vile, kuma wewe “
Alijibu potonto huku akiendelea kutembea.
Shadrack alimuangalia jinsi alivyokuwa anatembea kilevi levi , mavazi yake jinsi yalivyochoka na  hata sura yake , alikuwa anaonekana mkubwa kuliko yeye , lakini ukweli ni kwamba walisoma darasa moja toka shule ya msingi  na walikuwa marafiki wakubwa , walicheza michezo yote ya mtaani pamoja lakini alifeli shule ya msingi wakati shadrack alipo fauli shule ya kata japo hata yeye hakufanya vizuri zaidi lakini aliishika kusoma chuo cha kutunza nyumba. Na sasa yupo huko kusafisha nyumba za washua wakati mwenzake ndio kazi kushinda na mitungi kwenye virabu akibomu kila mtu aliyemjua mpaka kieleweke.
“oya pontonto  inakuaje mtu wangu wa nguvu , mbona umepotea hivyo kitaa nilifikiri umesafiri?”
Aliongea shadrack  huku akijifanya kuchangamka kinafiki.
“niende wapi mimi jembe langu  wakati dar ndio nyumbani.”
Aliongea potonto huku akiyumba yumba hivi kwa kurudi nyuma kwenda mbele.
“niambie mkali wangu mishe zina kwendaje?”
Shadrack aliongeza.
“mishe kitu gani mkali wangu , mishe mnazifanya nyie huko na washua, chakufanya nizungushie raundi hapa mimi nijimiminie mitungi barida.”
Aliongea  potonto kwa sauti ya kilevi levi .
Shadrackl hakutaka kufanya nae maongezi nae sana , aliingiza mkono wake mfukoni haraka na kutoa noti ya shilingi elfu tano na kisha kumdakisha.
“barida mkali wangu , ndio maana nakukubali shadrack wewe ndio jembe la maana.”
Aliongea potonto kwa furaha kinoma , lakini alivyochomoka hapo yani hata maongezi yenyewe na shadrack aliyakatisha, alirudi kirabuni akiwa na madaha kinoma , shadrack alimuangalia jinsi alivyokuwa anawasukuma sukuma walevi wenzie humo ndani aliishia kutikisa kichwa chake kwa  huruma kinoma.
“oya shadrack , shadrack na mimi nitoe mai tano ,”
Aliongea mlevi mmoja alikuwa amelala chali kwenye kichochoro hicho  suruali yake yote ikiwa imelowa kwa mkojo .
“embu  toka zako huko lpyana umejikojolea, pombe zitakuua wewe mjinga .”
Shadrack alifoka.
‘eeh na wewe shadrack nipe jero tu, nataka chupa moja tu ya mwisho, moja tu.”
Aliongea tena mvulana huyo na alafu safari hii alijamba  mavi yake yalikuwa yananuka kinoma.
“toka zako huko mwehu wewe.”
Alifoka  shadrack huku akimpita kwa kumruka pale chini sababu alikuwa amejilaza kwa kuziba kichocoro chote .
Watu wote walipita hapo ilikuwa lazima wamruke yeye.
MWISHO WA KITABU CHA KWANZA.
KWA VITABU ZAIDI WASILIANA NAMI KWA :
WHATSAP: +255 715 557 191
Tafadhari heshimu kazi ngumu ninayofanya, huruhusiwi kunakili na kupost simulizi yangu katika website, page wala whatsap group lako, stori zangu zote zimesajiliwa matumizi yoyote ya simulizi hii  bila idhini ya Gift kipapa ni kosa kisheria. 



NENDA KWNYE ORODHA YA VITABU.

No comments:

Post a Comment